Life imekuwa side quest na sijui main mission iko wapi
So leo nimeamka nikafeel kama niko ndani ya mchezo but sijui objective ni gani. Like unafanya vitu daily—unaamka, unaenda hustle, unarudi, unascroll, unalala… then repeat. Lakini ndani deep unajiuliza, “hii ndio ilikuwa plan kweli?”
Juzi nilikuwa kwa mat nikaskia watu wawili wakidebate kuhusu life—mmoja anasema pesa ndio kila kitu, mwingine anasema peace of mind ndio muhimu. Mimi niko hapo katikati nashangaa, bro mimi nataka zote mbili 😭
Na vile adulting huja na surprise attacks… bills zinatokea tu kama enemies kwa game. Hakuna warning. Hakuna tutorial. Just vibes and pressure.
Alafu kuna ile moment unacheki watu wako same age wako mbali sana life… mwingine ako abroad, mwingine ameanza biashara, mwingine amepata mtoto… wewe bado unadebate kama u-buy lunch ama ushinde na hunger kidogo u-save 200 bob.
Lakini kusema ukweli, maybe hakuna mtu anajua what they’re doing. Maybe sote tuna freestyle hii life. Some just look more confident doing it.
Anyway, kama uko hapo feeling lost kidogo, uko sawa. At least uko trying. Na hiyo yenyewe ni progress.
Sasa wacha nirudi kwa side quest zangu